UNAHITAJI MAFANIKIO YA KWELI?
Mbinu zifuatazo zitakusaidia kufikia mafanikio hayo.
Kuna tofauti kubwa sana kati yakuielewa falsafa na kuiishi falsafa.Falsafa ni mawazo ambayo huonekana ya maana pale tu yanapofanyiwa kazi na matokeo yakaonekana.Usiishie kuwaza/kufikiri pekee bali tenda yale unayoyawaza ndipo yatakuwa na msaada. (Msingi mhimu katika
maisha ni kuwaza na kutenda)
Kuna watu wengi sana ambao wanataka kutenda pasipo kuwaza na wengine wanawaza pasipo kutenda. Huyu anayetaka kutenda bila kuwaza unaweza jiuliza anatenda nini? Pengine anaweza tenda kile alichoamriwa na mwingine, hata hivyo hatakitenda sawasawa na jinsi kinavyotakiwa kuwa na matokeo yake kufanikiwa ni kidogo. Pi mawazo bila vitedo ni bure maana hayawezi kuleta matokeo yoyote. (Napenda mawazo mapya, napenda kufanya kazi)
Kama unataka mafanikio ya kweli anza kwa kuwaza na kutambua ni Nyanja gani unataka mafanikio(kiimani,kimahusiano,kikazi,kiuchumi,kisiasa au kwa jambo lolote lile ulilopanga). Weka mikakati ya kuweza kufikia hiyo hatua unayoitamani na kasha anza kuifanyia kazi hiyo mikakati yako. (usifanye kwa mazoea)
Wakati wa utekelezaji unatakiwa kuchunguza na kubaini ni mkakati ipi kati ya yote ulojiwekea imeanza kuonyesha dalili njema.Ile inayoonekana kuzaa matunda ndiyo ya kukazana nayo lakini kwa ile inayolegalega huna budi kuachana nayo maana itakuchelewesha.Usilazimishe kitu kimoja kikuleletee matokeo tofauti. ( Ujinga ni kufanya kitu kile kile huku ukitegemea matokeo tofauti)
Mhimu kuzingatia:-
1)Tafuta wazo jipya
2)Tafuta mtu yeyote aliyewahi kufanya hiko ulichowaza kufanya
3)Ongeza maarifa zaidi kwa aidha kusoma vitabu au kuhudhuria semina zinazohusiana na wazo lako
4)Tafuta eneo sahihi la kutekeleza wazo lako
5)Anza utekelezaji
Chief Mwinula
Chiefmwinula@gmail.com
Tumia fursa yako
Ongeza thamani yako