Sunday, 27 August 2017

FURSA

UTANGULIZI
Fursa ni nafasi ya kufanya jambo lolote lenye manufaa. (An opportunity is favourable time or set of circumstance of doing something) Chochote unachoweza kufanya na kikaleta manufaa ni FURSA.
Jambo lolote zuri huwa na manufaa pale tu mhusika anapoamua kulifanya kwa vitendo, na hii ndo maana halisi ya kutumia fursa.
Chanzo kikubw cha umaskini na kutofanikiwa katika nyanja mbalimbali kimaishi ni kutotumia vizuri fursa tulizonazo. (The big mistake in life is to let an ample opportunity lie dormant) Watu wengi wanashindwa kunufaika na fursa zao aidha kwa sababu hawazitambui au hawajui namna ya kuzitumia .

Karibu sana katika page hii tujifunze mengi juu ya na namna ya kutaua na kutumia fursa tulizonazo. 

Tuesday, 8 August 2017

ISHI KULINGANA NA FALSAFA YAKO

UNAHITAJI MAFANIKIO YA KWELI?

Mbinu zifuatazo zitakusaidia kufikia mafanikio hayo.

Kuna tofauti kubwa sana kati yakuielewa falsafa na kuiishi falsafa.Falsafa ni mawazo ambayo huonekana ya maana pale tu yanapofanyiwa kazi na matokeo yakaonekana.Usiishie kuwaza/kufikiri pekee bali tenda yale unayoyawaza ndipo yatakuwa na msaada.    (Msingi mhimu katika
maisha ni kuwaza na kutenda)

Kuna watu wengi sana ambao wanataka kutenda pasipo kuwaza na wengine wanawaza pasipo kutenda. Huyu anayetaka kutenda  bila kuwaza unaweza jiuliza anatenda nini? Pengine anaweza tenda kile alichoamriwa na mwingine, hata hivyo hatakitenda sawasawa na jinsi kinavyotakiwa kuwa na matokeo yake kufanikiwa ni kidogo. Pi mawazo bila vitedo ni bure maana hayawezi kuleta matokeo yoyote.   (Napenda mawazo mapya, napenda kufanya kazi)   

Kama unataka mafanikio ya kweli anza kwa kuwaza na kutambua ni Nyanja gani unataka mafanikio(kiimani,kimahusiano,kikazi,kiuchumi,kisiasa au kwa jambo lolote lile ulilopanga). Weka mikakati ya kuweza kufikia hiyo hatua unayoitamani na kasha anza kuifanyia kazi hiyo mikakati yako. (usifanye kwa mazoea)

Wakati wa utekelezaji unatakiwa kuchunguza na kubaini ni mkakati ipi kati ya yote ulojiwekea imeanza kuonyesha dalili njema.Ile inayoonekana kuzaa matunda ndiyo ya kukazana nayo lakini kwa ile inayolegalega huna budi kuachana nayo maana itakuchelewesha.Usilazimishe kitu kimoja kikuleletee matokeo tofauti. ( Ujinga ni kufanya kitu kile kile huku ukitegemea matokeo tofauti)

Mhimu kuzingatia:-

1)Tafuta wazo jipya

2)Tafuta mtu yeyote aliyewahi kufanya hiko ulichowaza kufanya

3)Ongeza maarifa zaidi kwa aidha kusoma vitabu au kuhudhuria semina zinazohusiana na wazo lako

4)Tafuta eneo sahihi la kutekeleza wazo lako

5)Anza utekelezaji

Chief Mwinula Chiefmwinula@gmail.com

Tumia fursa yako
Ongeza thamani yako